Jumatano 16 Septemba 2026 - 23:45
Mashindano ya Utafiti kwa Vijana katika Tawi la Al-Mustafa, Iraq

Hawza/ Tawi la Al-Mustafa nchini Iraq limendaa kwa wanafunzi vijana wa masomo ya Hawzah mashindano ya utafiti wa kielimu kwa vijana, yenye kaulimbiu isemayo “Shahidi Sayyid Ali Khamenei.”

Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Hawza, Hawzah Tawi la Al-Mustafa nchini Iraq inawaalika wanafunzi vijana kushiriki katika mashindano ya utafiti wa kielimu kwa vijana yenye kaulimbiu isemayo “Shahidi Sayyid Ali Khamenei.”

Mada kuu za mashindano hayo zinahusisha mwenendo wa jihadi na kisiasa wa Shahidi Khamenei, vipengele vya fikra na imani katika njia na mwenendo wa Shahidi Khamenei, pamoja na athari za Imam Shahidi kwa Umma wa Kiislamu na masuala yake ya kisasa.

Masharti ya kushiriki katika shindano hilo:

- Makala inapaswa kuwa na takriban maneno 1,500 na yasizidi maneno 3,000.
- Utafiti unapaswa kuandikwa kwa lugha fasaha na nyepesi ya Kiarabu.
- Makala inapaswa kutumwa katika mfumo wa PDF kupitia anuani ya barua pepe itakayowekwa hapa chini, huku ikiambatanishwa na jina kamili la mwandishi, namba ya simu na umri wake.

Kwa maelezo zaidi na mawasiliano na waandaaji:

07711145762

Kararalkafaje77@gmail.com

Mashindano ya Utafiti kwa Vijana katika Tawi la Al-Mustafa, Iraq

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha